Katika jitihada za kuboresha ustawi wa jamii na maendeleo ya wananchi, Afisa Maendeleo aliendelea kusikiliza changamoto zinazowakabili wananchi ili kutafuta njia bora za kuzitatua.
Wakati wa mkutano huu, wananchi walipata fursa ya kueleza matatizo yao, huku Afisa Maendeleo akisikiliza kwa makini na kutoa ushauri wa hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kuleta suluhisho la kudumu. Lengo kuu la kikao hiki lilikuwa kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata msaada unaostahili na kuimarisha maendeleo katika jamii.
Hatua hii ni sehemu ya jitihada za serikali za kusogeza huduma kwa wananchi na kuhakikisha kwamba changamoto zao zinashughulikiwa kwa wakati.
#MSLAC #KatibanaSheria #SSH #CCM #KaziIendelee #NchiyanguKwanza #SisiniTanzania #matokeochanya