Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Fatma Mwassa, ametoa wito kwa watumishi wa umma kutumia kampeni ya msaada wa kisheria kama sehemu ya kujifunza na kuboresha namna ya kushughulikia changamoto za wananchi.
Akizungumza kuelekea uzinduzi wa kampeni hiyo utakaofanyika Bukoba – Uwanja wa Mayunga, Mhe. Mwassa amesisitiza kuwa kampeni hii si tu kwa ajili ya kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi, bali pia ni darasa kwa watumishi kujifunza namna bora ya kuwahudumia wananchi kwa haki na usawa.
📍 Uzinduzi: Bukoba – Uwanja wa Mayunga
📅 Tazama video hii kwa maelezo kamili ya tarehe na ratiba
🎥 Sikiliza kauli ya Mhe. Fatma Mwassa na ujifunze umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika kampeni hii.
🔔 Subscribe kwa taarifa zaidi, penda video hii na washirikishe wengine.
#fatmamwassa #kampeniyakisheria #msaadawakisheria #kagera #bukoba #uwanjawamayunga #watumishiwaumma #habaritanzania