Skip to main content

Kata ya Kibilizi, Kigoma, imepokea msaada wa kisheria kupitia Mpango wa Msaada wa Kisheria wa Mama Samia (MSLAC), ukiongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria pamoja na timu ya wanasheria

Submitted by admin on 25 January 2025

Huduma hizi zimewalenga wananchi wa kipato cha chini kwa kuwapa elimu kuhusu sheria za ardhi, ndoa, mirathi, ukatili wa kijinsia, na mikataba ya ajira. Lengo kuu ni kuhakikisha wananchi wanapata haki zao na kutatua migogoro kwa njia ya amani na kwa mujibu wa sheria. Wananchi wameonyesha mwamko mkubwa, huku Waziri akisisitiza kuwa msaada huu utaendelea mara kwa mara.

#MSLAC #Katibanasheria #SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #SisiniTanzania #matokeochanya @samia_suluhu_hassan Ikulu Tanzania