Maafisa Maendeleo kutoka Dawati la Msaada wa Kisheria katika Halmashauri ya Wilaya ya Handeni wamefanikiwa kutembelea Kata ya Kwamsisi, hususan katika Vijiji vya Kwamsisi na Pozo. Ziara hiyo imelenga kutoa elimu ya msaada wa kisheria na kulitambulisha dawati hilo kwa wananchi, ili kuwasaidia kupata haki zao kwa urahisi.