Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akifuatilia uwasilishaji wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka 2025/2026, Bungeni Dodoma leo Jumatano Aprili 30, 2025. Wizara hiyo kupitia kwa Waziri Dkt. Damas Ndumbaro imeomba kuidhinishiwa Jumla ya shilingi 687, 698,489,000 kwaajili ya matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2025/26.
