Ujumbe huu unahimiza wananchi kutokaa kimya wanapokosa haki au wanapokutana na changamoto zinazohusu maisha yao ya kisheria na kijamii. Kukaa kimya ni kuruhusu kunyimwa haki, lakini kuzungumza na kudai ni hatua ya kwanza ya kuhakikisha haki inapatikana.
Kampeni hii inalenga kuwaelimisha wananchi wote kwamba Serikali kupitia Mama Samia Legal Aid Campaign ipo kwa ajili ya kuwasaidia bila malipo, kuhakikisha kila mmoja anapata msaada wa kisheria pale inapohitajika.
#WizaraYaKatibaNaSheria #HudumaKwaWananchi #MamaSamiaLegalAid #HakiKwaWote #HakiSawa #MsaadaWaKisheria #SheriaNiNguvu #ElimuYaSheria #SisiniTanzania #nchiyangukwanza #TanzaniaNiwajibuwetu #Nchiyetufahariyetu #kazinaututunasongambele