Waziri wa Katiba na Sheria Mheshiwa Dkt Damas Ndumbaro amewasili katika uwanja wa Stendi ya Zamani Kwa ajili ya Uzinduzi wa kampeni ya msaada wa Kisheria Ya Mama Samia Kwa Mkoa wa Morogoro.Ameanza Kwa kutembelea mabanda mbalimbali ya Taasisi zilizoshiriki katika uzinduzi wa kampeni hiyo.
Miongoni mwa mabanda hayo ni pamoja na ;
1.Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF )Tanzania.
2.Chuo Kikuu Cha Mzumbe
3.Tanzania paralegals Network (TAPANET)
4.Tanganyika Law Society (TLS)
5.Ofisi ya Wakili mkuu wa serikali
6.Wakala wa usajili,ufilisi na Udhamini(RITA)
7.Wizara ya katiba na sheria
8.Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mkoa wa Morogoro #KatibaNaSheria #Mslac #MsaadaWaKisheriaKwaHakiUsawaAmaniNaMaendeleo