Skip to main content

Waziri wa katiba na sheria Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi leo Novemba 19,2024 amekutana na kufanya mazungumzo na Shirika la Legal Service Facility kujadili mikakati ya uboreshaji utoaji haki na Msaada wa Kisheria kwa wanyonge kupitia kampeni ya Msaada

Submitted by admin on 19 November 2024
Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Kabudi amesema kuwa serikali inatambua mchango mkubwa unaofanywa na Legal Services Facility katika kuwezesha upatikanaji wa Haki kupitia Huduma za Msaada wa Kisheria kwa kuwawezesha Wasaidizi wa Kisheria kufika katika maeneo ya pembezoni na kuwapatia mafunzo hatua iliyopelekea huduma za Msaada wa Kisheria kuongezeka.
May be an image of 1 person and dais
Aidha kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Legal Service Facility Bi. Lulu Gw’anakilala amehaidi kuendelea kushirikiana na serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria kuwezesha Wasaidizi wa Kisheria kushiriki katika utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia kikamilifu ili kuhakikisha kampeni hiyo inakua mkombozi kwa wananchi wote hasa wasioweza kumudu huduma hizo.
May be an image of 1 person, newsroom and text
Wizara ya Katiba na Sheria imeendelea kusimamia masuala ya upatikanaji wa Haki Nchini ikiwa ni pamoja na kuratibu na kusimamia Huduma za Msaada wa Kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Msaada wa Kisheria Sura ya 21 ya Mwaka 2017, ambapo imeendelea kutekeleza jukumu la kusimamia na kuratibu utoaji wa huduma za msaada wa Kisheria nchini kwa kuhakikisha kwamba Mashirika ya watoa huduma za Msaada wa Kisheria yanatoa huduma iliyo bora kwa wananchi hususani wasiokuwa na uwezo.