Skip to main content

Arusha, Machi 1, 2025 – Wakazi wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa wingi kushiriki katika kampeni ya msaada wa kisheria iliyoanzishwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kampeni ambayo ilizinduliwa rasmi leo mkoani humo

Submitted by admin on 1 March 2025

Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Jumanne Sagini, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Paul Christian Makonda, waliongoza shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi. Kliniki za kisheria ziliwekwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa, ambapo wananchi walihudhuria kwa wingi na kupata fursa ya kushauriana na wataalamu wa sheria kuhusu changamoto zao, zikiwemo migogoro ya ardhi, mirathi, masuala ya kifamilia, na haki za kijinsia.

#sisinitanzania #maendeleo #tanzaniampya #sisinitanzaniampya #tanzaniayetu #tanzanianamaendeleo #tanzania #samiasuluhu #ssh #sisinitanzaniamakini #sisinitanzania #tanzaniabora #millardayo #updates #news #habari #habarimpya #news