Wamefanikiwa kutembelea ofisi za ardhi na kukutana na afisa ardhi wa halmashauri kwa ajili ya kufuatilia na kupata mrejesho wa migogoro ya ardhi ya wananchi iliyokuwa ikitafutiwa ufumbuzi. Pia, wamepata nafasi ya kutambulisha dawati la msaada wa kisheria kwa mkuu wa Idara ya Ardhi na baadhi ya watumishi wa idara ya ardhi ya halmashauri. Hakika tunaona umuhimu wa huduma ya msaada wa kisheria kwani imekuwa msaada kwa wananchi kutambua haki zao kikamilifu.
#MSLAC #KatibanaSheria #SSH #CCM #KaziIendelee #NchiyanguKwanza #SisiniTanzania #MatokeoChanya