Skip to main content

MSLAC Yatoa Elimu ya Msaada wa Kisheria kwa Wajasiriamali Katika Mnada wa Kijiji cha Mlogolo, Wilaya ya Sikonge

Submitted by admin on 9 January 2025

Kijiji cha Mlogolo kilichopo katika Wilaya ya Sikonge kimeandika historia mpya baada ya kupokea elimu ya msaada wa kisheria kupitia kampeni ya Samia Legal Aid Campaign (MSLAC). Elimu hii ilitolewa wakati wa mnada maarufu unaowakutanisha wakazi wa vijiji mbalimbali vya Sikonge, lengo likiwa ni kuwawezesha wajasiriamali wadogo na wa kati kufahamu haki zao za kisheria na taratibu zinazopaswa kufuatwa katika shughuli zao za kibiashara.

Mnada wa Mlogolo, ambao unajulikana kwa kuwa kiunganishi kikubwa cha wafanyabiashara wa mazao, mifugo, na bidhaa nyingine za nyumbani, uligeuka kuwa jukwaa la mafunzo ya kisheria. Washiriki walipata fursa ya kujifunza masuala muhimu kama haki za mikataba ya kibiashara, taratibu za kukopa fedha kupitia taasisi za kifedha, umuhimu wa kuweka kumbukumbu sahihi za biashara, pamoja na namna ya kushughulikia migogoro inayoweza kutokea kwenye mazingira ya kibiashara. 

#MSLAC #Katibanasheria #SSH #CCM #KaziIendelee #Nchiyangukwanza #SisiniTanzania #matokeochanya @samia_suluhu_hassan @ikulu_mawasiliano @dr_philip_isdor_mpango @biteko

@katibanasheria_ @profkabudipjam @Victoria

.mwanziva @tanganyikalawsociety @boniface_a_k_mwabukusi